Consulting

To monitor implementation and principle of cultural accountability within CSO’s to ensure accountability, efficiency and effectiveness so as to meet the organization objectives.

A Platform

Act as platform for collecting, analysing and dissemination of the information that could help to meet the objectives and purpose of the NGO’s members as well as exchanging information with other stakeholders.

Specific Objective

To Coordinate Civil Society Organizations based in Pemba Island.

A Trainer

To provide capacity building skills to NGO members

24 May, 2024

Elementor #142

PACSO KUPITIA MRADI WA URAIYA WETU WANAWAPATIA MAFUNZO AFSA USTAWI WA JAMII

17 Nov, 2023

PACSO: ‘TUNATEKELEZA KWA VITENDO MAONO YA DK. MWINYI, DK. SAMIA’

MRATIBU wa miradi kutoka Mwenvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema wanatekeleza kwa vitendo, maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, la kuhakikisha elimu ya uraia na demomkrasia inawafikia wananchi.

Mratibu huyo aliyasema hayo, wakati akizungumza na watendaji wa serikali na wanaasasi za kiraia, katika kongamano la pamoja, la kujenga ushirikiano, baina pande mbili hizo, kupitia mradi wa ‘uraia wetu’ lililofanyika Wawi Chake chake.

Alisema, mradi huo ni tokeo moja wapo la maono ya viongozi hao, ambapo wameamua kuwakusanya watendaji wa serikali na wale wa asasi za kiraia, ili kuibua changamoto zinazokwamisha ushirikiano wao.

Alieleza kuwa, washiriki wa kongamanio hilo, watapata nafasi ya kuelezea changamoto zao kikanuni, sera na kisheria ili kuona zinatatuliwaje kwa umoja wao.

‘’Sote ni mashahidi kuwa, wakati viongozi wetu wanaingia madarakani, walihimiza mno suala la kuzifahamu sheria, kuona changamoto zake na hata kuzifanyia marekebisho, ili kusiwe na mkwamo katika utekelezaji wa shughuli husika,’’alieleza.

Aidha Mratibu huyo wa miradi kutoka ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alieleza kuwa washiriki watachambua sera, kanuni na sheria ambazo wakati wanapotekeleza majukumu yao, zinawakwaza.

 

 

Katika hatua nyingine alifafanua kuwa, PACSO imeandaa jukwaa la kuwakutanisha pamoja watendaji wa serikali na wanaasasi za kiraia, ili kujadili kwa pamoja changamoto za watu wenye ulemavu, vijana na wanawake.

Alieleza kuwa, maoni ambayo yatapatikana katika kongamano hilo, watayaandika vyema na kuyasilisha kwa Jumuiya ya wanawake wanawake wenye ulemavu Zanzibar, ambao nao watakeleza mradi kama huo, ngazi ya kitaifa.

‘’Kwenye mradi huu PASCO, inatekeleza ngazi ya kanda (zone), ingawa wenzetu wa JUWAUZA wanatekeleza ngazi ya kitaifa na kisha maoni hayo, watayafikisha kwa viongozi wa kitaifa,’’alieleza.

Akifungua kongamanio hilo, Msaidizi Naibu Mrajisi wa Asasi za Kiraia Pemba, Saada Abubakar Khamis, alisema mradi huo, unaweza kuleta tija, kwa vile unaangalia kwa upana wake, suala la demokrasia.

Alieleza kuwa, moja ya chanagamoto iliyopo ni kutoonekana kwa uhusiano mzuri, baina ya asasi za kiraia na serikali kuu, jambo ambalo wakati mwengine huchelewa kutekelezwa kwa miradi.

‘’Jambo hili lililofanywa na wenzetu ‘PACSO’ naamini litazidisha ushirikiano na uhusiano mzuri uliopo baina ya serikali na asasi za kiraia, hasa kwa vile pia litaangalia sheria na kanuni zinazokwamisha utendaji wa asasi,’’alifafanua.

Alifafanua kuwa, demokrasia ni dhana pana na wakati mwengine wapo wanaoona inahusu ngazi za juu pekee, bila ya kuona kuwa dhana hiyo, hutakiwa kuonekana hata kwenye asasi za kiraia.

Wakichangia kwenye kongamano hilo, washiriki hao walisema ushirikishwaji ni jambo jema, katika kufikia uamuzi wowote, katika nchi ama asasi za kiraia.

Afisa wa watu wenye ulemavu wilaya ya Chake chake Mwadini Ali Juma, alisema bado watu wenye ulemavu, hawajatendewa haki sana katika ajira, miundombinu na majengo ya umma.

Mwakilishi kutoka TAMWA, Asha Mussa Omar, alisema kikwazo kilichopo ni kwa jamii, kutotaka kubadili mitazamo, juu ya dhana ya mwanamke na uongozi.

‘’Wapo baadhi ya watu wanawavunja moyo wanawake, kwa kuwaambia kuwa wakiwa viongozi, watakuwa wamevunja maadili, watapewa takala, dhana hizi zinahitaji elimu kwa bidii,’’alieleza.

Akiwasilisha mada ya umuhimuwa ushirikiano baina ya asasi za kiraia na serikali, mkufunzi Juma Bakar Alawi, alisema hakuna haja ya pande mbili hizo, kunyimana taarifa.

Alieleza kuwa, asasia zote za kiraia Zanzibar, zinatekeleza miradi ambayo ni maono ya serikali kuu, hivyo ni vyema pande moja wapo inapohitaji taarifa, iwe rahisi kupeana.

Kongamano hilo la siku moja, kupitia mradi wa ‘uraia wangu’ limeandaliwa na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society kupitia Umoja wa nchi za Ulaya.

10 Oct, 2023

JAMII YAKUMBUSHWA KUILINDA HAKI KUU YA BINAADAMU

JAMII imekumbushwa kuwa, moja ya haki kuu ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni kosa kwa mtu mwengine yeyote kumuondolea mwenzake.

Hayo yalielezwa na mtoa mada mwanasheria kutoka Shirika la Msaada na Haki za Binaadamu Siti Habib Mohamed, wakati akiendesha mafunzo ya siku nne kwa waandishi wa habari, wadau wa habari na wasaidizi wa sheria, yanayofanyika Chuo cha Amali Vitongoji Chake chake na kuandaliwa na Mwemvuli wa asasi za Kirai Pemba PACSO kwa ufadhili wa UNDP.

Alisema kua zana ya haki za binadamu ilianzishwa mnamo  mwaka 1948 baada ya vita vya kwanza vya dunia, hivyo ni wajibu wa kila mmoja hadi leo hii, kuhakikisha anailinda na kuitetea haki ya kuishi ya mwanzake.

Alieleza kuwa, haki za binadamu kimsingi ni yale madai au haki zote ambazo anadai binamu mara baada ya kuzaliwa, na kwa kawida hakuna taasisi yoyote ambayo inaweza kuzuia.

‘’Ni kweli haki ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha anailinda yake mwenyewe na mwenzake,’’anaelkeza.

Hata hivyo alieleza kua kupitia Mkataba wahaki za  binadamu ambao uliasisiwa mwaka 1966 na kuanza kufanyaka kazi mwaka 1976, umeanisha haki nyingine kadhaa za binadamu kama vile kutoa maoni.

Katika hatua nyingine mtoa mada huyo alieleza kua zipo hatua mbali mbali, ambazo zimekuja kwa ajili ya kuzilinda haki hizo ikiwa ni pamoja na kuanzishwa wizara maalum, kuanzishwa kwa tume ya Haki za binadamu na utawala bora.

‘’Lakini hata kuingizwa kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na ile ya Zanzibar ya mwaka 1894 na uwepo wa wizara husika na asasi ni sehemu ya kuzilinda,’’alifafanua.

Mapema Mkurugenzi wa PACSO Mohamed Najim Omar, alisema waliona wakutane na waandishi wa habari, wanaharakati wa haki za binadamu na wasaidizi wa sheria, ili kuwajengea uwezo.

‘’Waandishi wananafasi kubwa ya kuhakikisha wanakemea matendo ya uvunjifu wa haki za binadamu kupitia kazi zao,’’alieleza.

Washiriki wa mafunzo hayo walisema bado elimu inahitajika kwa jamii, ili wafahamu athari za uvunjifu wa haki za binadamu.

Mshiriki kutoka chama cha ACT Wazalendo Saleh Nassor Juma, waliishukuru taasisi hii ya PACSO kwa kuwapa mafunzo hayo, ambayo yamewapa uwelewa zaidi.

Nae mtaangazaji wa Redio Istiqama Pemba Bakar Khamis Juma, alisema kama mataifa makubwa, yatajenga utamaduni wa kuziheshimu haki za binadamu dunia itakuwa salama.

Nao washiriki Abubakar Mohamed Ali ,Mwache Juma Abdalla walisema, kama vyombo vya habari vitakuwa huru kufanya kazi, wanaweza kukemea matendo ya uvunjifu wa haki za binadamu yanayojitokeza.

Mratibu wa miradi kutoka Shirika la Maendeleo Ulimwenguni la UNDP Gamalick Sun  alisema wataendelea kuiunga mkono PACSO katika shughuli zao mbali mbali.

Alieleza kuwa, anaamini PACSO ni sehemu ya uwakilishi wa wananchi, na ndio maana hata mafunzo hayo yamewashirikisha watu wa kada mbali mbali.

Mafunzo hayo ya siku nne mada kadhaa zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na uhuru wa kujieleza, haki za binaadamu, majukumu ya waandishi wa habari na jukumu la jamii katika kulinda haki za binaadamu,.